Bumbuli ni moja ya vijiji vya zamani sana katika nchi ya Tanzania.
Kiongozi wa jadi aliyekuwa anaongoza Bumbuli kabla ya uhuru alikuwa
anaitwa Zumbe
Daudi Sozi Kibanga Moja ya sifa za kiongozi huyu ilikuwa kuleta mvua,
tofauti na viongozi wa makabila mengine Zumbe Daudi Sozi Kibanga alikuwa
haleti mvua kwa njia ya uganga au uchawi la hasha. Zumbe Daudi alikuwa
na kipawa cha kuomba (sala) kwa mwenyezi Mungu na wananchi wakapata
mvua. Mahali alipokuwa anakaa Zumbe Daudi palikuwa panaitwa Kitaa. Kabla
ya kuja Wamisionari wa Kwanza wa Kijerumani katika eneo hili kijiji
kilikuwa kimoja kinachoitwa Kungutana.
Baada ya kuja Wamisionari wa Kwanza wa Kijerumani walivutiwa sana na
eneo hili ndipo walipowashawishi wananchi kuhamia maeneo mengine ili
waweze kujenga Kanisa na shule katika eneo hilo la Kungutana. Wananchi
wa eneo hilo walihama eneo hilo na wengi walihamia kijiji kinachoitwa
Bumbuli Kaya, mita 200 tu kutoka Kungutana na wengine walihamia eneo
jipya linalojulikana kama Bumbuli Mission. Wamisionari wa Kijerumani
walijenga shule mbili na Kanisa. Shule ya Maduda ambayo ilikuwa middle
school kwa wakati huo. Na nyingine inaitwa Shule ya Msingi Bumbuli na
Kanisa la Kilutheri lipo mpaka leo.
Wajerumani hawa waliendelea na kujenga hospitali kubwa sana katika
eneo hilo na kwa sababu wamisionari hawa wa Kijerumani walikuwa
Walutheri basi baada ya uhuru hospitali hiyo haikutaifishwa na serikali
kama uliokuwa mfumo wa wakati huo wa kutaifisha mashirika binafsi bali
ilipewa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini
Mashariki ili liendelee kuiendesha. Hospitali hiyo inaitwa Bumbuli hospitali.
No comments:
Post a Comment